Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, lini Serikali itafunga laini ya pili ya umeme kutoka Geita hadi Sengerema ili kutatua tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, sasa kwa kuwa Serikali imeamua kuchukua hatua hizo ni namna gani imejipanga ili tatizo hili lisitokee tena na kuathiri upatikanaji wa umeme kwenye maeneo ya Sengerema kama ilivyokuwa mwanzo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, kwa kuwa bado kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme kwenye maeneo ya visiwa vya Ukerewe na hasa kwenye maeneo ya visiwa vidogo ambako wanategemea umeme wa jua. Ni lini Serikali sasa itaondoa moja kwa moja matatizo ya umeme kwenye maeneo ya visiwa vidogo ya Visiwa vya Ukerewe?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu masala mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mkundi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la awali, kwamba mara baada ya tatizo hili kutokea Serikali ilikuwa inaipatia Sengerema umeme kutoka Kituo cha Mpovu kilichopo Geita. Mpango wetu wa pili sasa ni kuweka waya kupitia kwenye daraja badala ya kupitia chini ya maji ili vilevile Sengerema ipate umeme kutokea Mwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimhakikishie kwamba, pamoja na kwamba, lilitokea tatizo hili, lakini sasa imekuwa ni bahati kwao kwa watu wa Sengerema. Kwamba, sasa watakuwa na njia mbili za uhakika za kupata umeme. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba, umeme kwa Sengerema itakuwa tatizo hilo limeondoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na hili la kukatikakatika kwa umeme katika maeneo ya visiwa, Serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba maeneo yetu ya visiwa yanapata umeme wa uhakika. Pale ambapo teknolojia ya solar inaweza kutupatia umeme huo, tutatumia teknolojia ya kisasa kuhakikisha kwamba umeme unapatikana. Pale ambapo mazingira yataruhusu kupata umeme kutoka kwenye gridi, Serikali itafanya hivyo.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, lini Serikali itafunga laini ya pili ya umeme kutoka Geita hadi Sengerema ili kutatua tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, mkandarasi anayejenga Mradi wa Umeme Kijiji cha Kigurunde na Kijiji cha Makanka amechelewesha mradi ule sasahivi ni zaidi ya miezi sita.

Je, nini kauli ya Serikali juu ya mkandarasi huyu kuchelewesha mradi ule?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Shekilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inapenda kurudia kauli yake na maelekezo kwa wakandarasi, kwamba wanapaswa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ya kupeleka umeme kama ambavyo tumekubaliana nao kwenye mikataba. Mkandarasi yeyote ambaye atashindwa kutimiza wajibu wake aelewe kwamba, amejihakikishia, kwamba hatutampatia tena kazi katika nchi yetu. (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, lini Serikali itafunga laini ya pili ya umeme kutoka Geita hadi Sengerema ili kutatua tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara?

Supplementary Question 3

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa kuwa Serikali iliweka mkakati wa kukarabati mitambo na njia za umeme, ili kumaliza tatizo la katakata ya umeme na migawo ya umeme.

Je, tangu programu hiyo ilivyoanza mwaka 2022 Serikali imeweza kupunguza kwa kiasi gani katakata na migawo ya umeme inayoendelea wakiwemo wananchi wangu wa Jimbo la Kisesa?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya ya teknolojia huwezi kuwa na uhakika wa asilimia mia moja. Mambo haya ya umeme tatizo linaweza kutokea wakati wowote, unaweza kufanya matengenezo leo, kesho likatokea tatizo umeme ukakatika. Niombe tu aendelee kuiamini Serikali kwamba, tutajitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuhakikisha tunaondokana na matatizo haya. (Makofi)