Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 150 2024-02-09

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, lini Halmashauri ya Morogoro Vijijini na Rufiji zitalipwa fedha za CSR kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu kidogo cha 2.1.1 cha Mkataba wa Utekelezaji wa Miradi ya Kijamii uliosainiwa tarehe 12 Desemba, 2018 kati ya TANESCO na Mkandarasi, unaainisha kwamba, hakutakuwepo na malipo ya fedha taslimu yatakayofanyika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kijamii bali Mkandarasi atakabidhi miradi akikamilisha utekelezaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na Mkandarasi imepanga kujenga Hospitali mbili za hadhi ya Wilaya katika Kata ya Kisaki, Wilaya ya Morogoro Vijijini na Kata ya Nyamwage, Wilaya ya Rufiji zenye gharama ya shilingi bilioni kumi kila moja. Kwa sasa Serikali imekamilisha maandalizi ya nyaraka za msingi ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hizo. Aidha, majadiliano kati ya TANESCO na Mkandarasi yanaendelea kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.