Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 152 2024-02-09

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na kuimarisha soko la bidhaa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali kwenye sekta ya kilimo kwa nia ya kuongeza tija kwenye uzalishaji kupitia uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji, pembejeo, utafiti, huduma za ugani, matumizi ya sayansi na teknolojia na kurasimisha sekta ya kilimo mazao. Serikali kupitia Soko la Bidhaa inaendelea kutoa elimu kwa wakulima na wadau kuzalisha kwa tija na kuuza katika soko rasmi (Soko la Bidhaa Tanzania) ambalo linawakutanisha na wanunuzi wakubwa wa nje na wa ndani na kuwapatia bei zenye ushindani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali inaendelea kuhamasisha kilimo cha kibiashara kinachozingatia mahitaji ya soko, kushiriki makongamano na maonesho ya kibiashara na uwekezaji kwa lengo la kutangaza bidhaa na maeneo ya uwekezaji katika sekta ya kilimo, kushirikiana na sekta binafsi katika ujenzi wa miundombinu ya masoko, kuimarisha mifumo ya kielektroniki ikiwa ni pamoja na kuanzisha kituo rasmi cha Intelijensia ya Masoko ya Mazao ya Kilimo (Agricultural Market Intelligence and Data Centre), ambayo itawezesha upatikanaji wa taarifa za masoko kwa wakati, kutoa mafunzo kuhusu kilimo biashara kwa Maafisa Ugani na wakulima na kuendelea kufungua masoko mapya katika nchi mbalimbali kwa kufanya tafiti za mahitaji kwa nchi husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali kupitia soko la bidhaa inaendelea kutoa elimu kwa wakulima na wadau kuzalisha kwa tija na kuuza katika soko rasmi ambalo linawakutanisha wanunuzi wakubwa wa nje na wa ndani na kuwapatia bei zenye ushindani. (Makofi)