Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 154 2024-02-09

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Nyashimo – Ndutwa – Shigala – Malili hadi Ngasamo itajegwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), tayari imekamilisha taratibu za zabuni kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri atakayefanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Nyashimo – Ndutwa – Shigala – Malili hadi Ngasamo yenye urefu wa kilometa 48. Mkataba wa Mhandisi Mshauri unatarajiwa kusainiwa mwishoni mwa mwezi Februari, 2024 na kazi ya usanifu inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2024. Baada ya kazi hiyo kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante.