Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 155 2024-02-09

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaacha kuwafukuza na kuwavunjia vibanda wajasiriamali wanaofanya biashara barabara kuu ya Segera – Korogwe – Moshi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la kuondoa vibanda vilivyojengwa kwenye eneo la hifadhi ya barabara kwa barabara kuu za Mkoa wa Tanga ikiwemo ile ya Segera – Korogwe – Moshi, lilifanyika kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007 ambayo inapiga marufuku uwekaji wa miundombinu yoyote kwenye eneo hilo bila idhini ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Hivyo, TANROADS ilibomoa vibanda vya wafanyabiashara ambavyo havikupangwa kwa mpangilio mzuri na kuwepo na vibali na TANROADS. Wale ambao walikuwa na vibali na vibanda vyao kupangwa vizuri hawakuondolewa, ahsante.