Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Questions to Prime Minister Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge 211 2024-02-15

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza: -

Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Nachingwea?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amandus Julius Chinguile, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Ibara ya 75 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, imeipa mamlaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kuchunguza na kugawa mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi katika Jamhuri ya Muungano mara kwa mara na angalau kila baada ya miaka kumi baada ya kupata kibali cha Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, katika maandalizi ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatangaza utaratibu na sifa za kugawa maeneo mbalimbali kwa ajili ya uchaguzi. Hivyo, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge, kuwa mara Tume itakapotangaza kugawa au kubadili majina ya Majimbo ya Uchaguzi, awasilishe ombi lake la kuligawa Jimbo la Nachingwea kwa kuzingatia utaratibu utakaotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Ahsante.