Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Nachingwea?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi na naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Jimbo la Nachingwea ni kubwa sana na lina kata ambazo zinapakana na Mkoa wa Morogoro lakini na Mkoa wa Ruvuma, Serikali pamoja na huo utaratibu haioni sasa ipo haja ya kugawanya maeneo ya kiutawala ili angalau kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Jimbo la Ndanda, limetawanyika pia kuelekea Mkoa wa Ruvuma, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Ndanda, ina sababishia wananchi watembee zaidi ya kilometa 80 kufuata huduma za Serikali. Je, Serikali haioni haja pia ya kugawa Jimbo hilo na kupatia halmashauri nyingine? (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Agnes Hokororo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la kuongeza Maeneo ya Utawala nilikuwa namshauri Mheshimiwa Mbunge, aendelee kuwasiliana na wenzetu wa TAMISEMI, kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa, Mamlaka, Wilaya sura ya 287 na kifungu cha 87(a)(1)(2) cha Sheria za Mamlaka za Serikali za Mitaa, kama zilivyorekebishwa katika marekebisho ya Sheria mbalimbali ili waweze kufuata huo utaratibu wa kuanzia u-DC, DCC, RCC na baadaye kuja Taifa ili waweze kuona namna ya kuzingatiwa kipindi hiko ambacho TAMISEMI, watafanya jambo hilo.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili. Kuhusu Jimbo la Ndanda, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi kwa mujibu wa Ibara ya 75 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tume imepewa mamlaka. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge, muda utakapofika Tume itakapotangaza basi na yeye afuatae utaratibu huo ambao utawekwa na Tume ili kusudi kuona jambo hilo utekelezaji wake, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza: - Je, lini Serikali italigawa Jimbo la Nachingwea?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwenye jibu la msingi, Waziri anasema Mbunge, aombe, mimi naamini kunakuwa kuna timu ya kufanya utafiti kutokana na vigezo. Hiyo habari ya Wabunge kuomba unakuta maeneo mengine yanagawanywa kisiasa, linaitwa Jimbo la Mjini, lina kata saba vijijini mwisho wa siku linaleta athari kwenye Mipango Miji ya maendeleo kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, ni vigezo gani vya msingi ambavyo mnavitumia ili kuhakikisha jimbo linagawanywa kwa ajili ya kuleta maendeleo ya wananchi?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nilipokuwa natoa maelezo yangu ya awali nilisema Mbunge aombe, maana yake ni baada ya Tume kuweka ule utaratibu sasa utafanya uweze kuomba, lakini vigezo naomba nivitaje kama ifuatavyo: -

(i) Ukubwa wa Jimbo husika, unaangaliwa;
(ii) Mipaka ya kiutawala;
(iii) Hali ya kiuchumi kama inaturuhusu;
(iv) Hali ya Kijiografia;
(v) Upatikanaji wa mawasiliano;
(vi) Jimbo lisiwe ndani ya Halmashauri au Wilaya mbili; na
(vii) Kata moja isiwe ndani ya Majimbo mawili.

Mheshimiwa Spika, lakini lipo sharti lingine la Ofisi yako ya Bunge, kutuambia kama tunayo nafasi humu ndani yakuendelea ku-accommodate idadi kubwa zaidi ya Wabunge. Kwa hiyo, nimetaja kwa uchache naomba niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge, muda utakapofika Tume ikitangaza basi vigezo na masharti vitakavyowekwa vitatuongoza kuona kwamba Jimbo hili linafaa kugawa au halifai, ahsante. (Makofi)