Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 213 2024-02-15

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Anania Tadayo, Mbunge wa Jimbo la Mwanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya Vituo vya Afya Vikongwe vinavyohitaji ukarabati. Hadi kufikia Disemba, 2023 jumla ya vituo vya afya 202 chakavu vimeainishwa kote Nchini kikiwemo Kituo cha Afya Lang’ata ambapo vitatengewa bajeti kwa ajili ya ukarabati kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na Vituo vya Afya Chakavu, pia ziko Hospitali Kongwe 50 za halmashauri zilizofanyiwa tathmini, na hospitali 38 zimeshapelekewa jumla ya shilingi bilioni 34.2 kwa ajili ya ukarabati katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 na 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, Serikali itatoa kipaumbele cha ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata katika bajeti zijazo, ahsante.