Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa kituo hiki kilijengwa takribani miaka 40 iliyopita na hakuna ukarabati wowote ambao umewahi kufanyika kiasi kwamba mpaka sasa hivi vyoo vimefungwa. Na kwa kuwa, eneo hili ni eneo la uvuvi na lina watu wengi sana na halina majisafi na salama kwa hiyo lina magonjwa mengi. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuidhinisha angalau milioni 100 za dharura ili kuondokana na changamoto hii inayotishia afya za watu?

Mheshimiwa Spika, swali la pil, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, yuko tayari baada ya Bunge hili tuongozane akajionee mwenyewe hali ya kile Kituo cha Afya ili aone umuhimu wa kutoa hizo fedha za dharura, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kwa namna ambavyo amefuatilia suala la Kituo cha Afya cha Lang’ata, lakini tulishamuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mwanga, kwamba Kituo cha Afya ni sehemu nyeti sana na sio rahisi kuruhusu Kituo cha Afya kisiwe na vyoo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nitumie fursa hii kumkumbusha na kumuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mwanga, mapema iwezekanavyo atenge pesa za dharura kwenye mapato ya ndani wajenge vyoo, Kituo cha Afya kiwe na vyoo wananchi wapate huduma bora. Na sisi tutafuatilia kwa sababu hili ni jambo muhimu sana na ni changamoto kuwa na Kituo cha Afya ambacho hakina vyoo.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, nipo tayari kufuatana na Mheshimiwa Mbunge, kwenda Mwanga kwa ajili ya ziara lakini ninaamini wakati tunakwenda tutakuta tayari vyoo vimejengwa na wananchi wanapata huduma bora za afya katika eneo hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Sisi Namtumbo, tuna Vituo vya Afya vitatu, Kituo cha Afya cha Mkongo, Kituo cha Afya cha Lusewa na Kituo cha Afya cha Mputa vilivyojengwa miaka ya 70 na vimechoka kabisa na havina vyumba vya upasuaji wala Wodi za kina Mama na Watoto. Je, Serikali imeweka katika list ya hivyo vituo chakavu na ambavyo vitafanyiwa ukarabati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nimhakikishie Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Kaka yangu Mheshimiwa Vita Kawawa, kwamba ameshawasilisha yeye mwenyewe vituo hivi vitatu na ameshaeleza kwamba ni vituo vikongwe na sisi tumeshatuma timu zetu zimefanya tathmini ni kweli havina baadhi ya majengo muhimu kama Majengo ya Upasuaji, Majengo ya Afya ya Mama, Baba na Mtoto na majengo mengine.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie ni miongoni mwa vituo ambavyo vimeingia kwenye orodha ya ukarabati na mara tukipata fedha tutahakikisha tunatoa vipaumbele kwa ajili ya ukarabati wa vituo hivyo, ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, Kituo cha Afya kilichopo Ikungwe, Jimbo la Kalenga kimekamilika lakini kuna changamoto ya waganga pamoja na vifaatiba. Ni lini Serikali itapeleka vitu hivyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Kituo cha Afya cha Ikungwe, ambacho Mheshimiwa Mbunge, amekisemea hapa ni kweli kimekamilika, lakini nimhakikishie tu na nina uhakika yeye ni shuhuda kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya mapinduzi makubwa sana katika, kwanza kuajiri Watumishi wa Sekta ya Afya.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka hii mitatu Serikali imeajiri Watumishi wa Afya 18,878 lakini imeshapeleka vifaatiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 300. Nikuhakikishie kwamba kituo hiki kipo kwenye orodha na tutapeleka watumishi lakini pia tutapeleka Vifaatiba, kwa ajili ya kuboresha Huduma za Afya, ahsante.

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Supplementary Question 4

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Wananchi wa Kata ya Kinyagigi Jimbo la Singida Kaskazini wamejitolea nguvu zao na kuweza kujenga kituo cha afya, kwa maana ya jengo la OPD na baadhi ya majengo, lakini bado kunahitaji gharama za ukamilishaji ambazo ni shilingi milioni 100.

Je, Serikali sasa haioni haja ya kuwasaidia wananchi hawa ili kumaliza jengo hilo ili kituo hicho kianze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza niwapongeze Wananchi wa Kata ya Kinyagigi ambao wamejitolea nguvu zao na kujenga majengo haya. Nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itatafuta fedha aidha kupitia mapato ya ndani ya halmashauri au Serikali kuu kwa ajili ya kupata hii milioni 100 kwa ajili ya kukamilisha majengo hayo.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Lang’ata – Mwanga?

Supplementary Question 5

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Umbwe hakina maabara, OPD na mortuary.

Je, ni lini Serikali itajenga vitu hivyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, vituo vingi vya afya hapa nchini hasa vile vilivyojengwa miaka ya nyuma vina upungufu wa baadhi ya majengo. Ndiyo maana Ofisi ya Rais TAMISEMI imefanya mapping ya vituo vyote kote nchini na kuvitambua vituo ambavyo vina majengo pungufu ya yale ambayo yanahitajika kwa ajili ya vituo vya afya kikiwemo kituo hichi cha Umbwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vituo hivi pamoja na hiki kituo kipo kwenye mpango na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuongeza majengo hayo ili viwe na majengo ili viwe na majengo yale yanayohitajika kwa ngazi ya kituo cha afya.