Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo 216 2024-02-15

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaboresha uwanja wa michezo katika eneo la Polisi Himo?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inayo nia ya dhati kuhakikisha kwamba uboreshaji wa miundombinu ya michezo nchini unafanikiwa ili kukuza ushiriki wa michezo na kuibua vipaji. Katika kufanikisha suala hili, Serikali imekuwa ikiwahimiza wamiliki wa viwanja na wadau mbalimbali wa michezo kushiriki katika kujenga na kuboresha miundombinu ya michezo katika maeneo mbalimbali nchini kama Sera ya michezo inavyoelekeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali inahimiza wamiliki wa uwanja wa michezo wa Polisi Himo kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta binafsi katika kuboresha uwanja huo. Aidha, Wizara ipo tayari kutoa ushauri wa kitaalam kwa wamiliki na wadau wanaokusudia kujenga ama kuboresha miundombinu ya michezo nchini.