Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha uwanja wa michezo katika eneo la Polisi Himo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, inaonekana kwamba Serikali haina mkakati madhubuti wa kujenga viwanja kwenye maeneo ya vijiji na maeneo mengine nchini. Naomba niulize maswali mawili mengine ya zaida.

Swali la kwanza, je, endapo tutaweza kuhamasisha wananchi wetu pale Himo ambapo kusema kweli kwenye Jimbo letu hatuna kiwanja chochote tukasawazisha, Serikali itakuwa tayari kutupa support ya nyasi bandia?

Swali la Pili, ni kwamba tunajua Serikali sasa inaingia kwenye mitaala mipya ya elimu ambapo tunahamasisha mkondo wa amali na michezo ni mmojawapo, hili halitafanikiwa kama kwenye maeneo tunayoishi hakuna sehemu za kufanyia michezo ya aina mbalimbali na kukuza stadi zetu.

Je, Serikali inaweza kutoa kauli gani kuhusiana na suala hili zima la kusaidia kukuza stadi za michezo mbalimbali kwenye maeneo yetu? (Makofi)

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge Dkt. Charles Kimei kwa swali ambalo halina maslahi na manufaa kwa vijana na wanamichezo kwa ujumla wa Jimbo la Vunjo na Mkoa wa Kilimanjaro pekee yake bali kwa nchi nzima. Namshukuru kwa moyo huo wa kiuanamichezo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inayo nia thabiti ya kujenga, kukarabati na kuboresha miundombinu mbalimbali ya michezo. Mheshimiwa Mbunge atakuwa anafahamu mipaka mizito ya kibajeti ambayo Wizara yetu inayo lakini tunaendelea kuwasiliana na wenzetu wa Wizara ya Fedha kuona namna ambavyo tunaweza kuongezewa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali ina mpango wa kukarabati viwanja saba vikubwa vya michezo nchini vikiwemo viwanja vya Jamhuri wa Morogoro, Jamhuri wa Dodoma, Sokoine wa Mbeya, Majimaji wa Songea, Mkwakwani Tanga na vinginevyo ili kuhakikisha tunakuwa na maeneo thabiti kabisa ya kufanya shughuli za michezo katika Mikoa husika.

Mheshimiwa Spika, hali kadhalika, kwa sasa Serikali imechagua shule 56, shule mbili katika kila Mkoa wa Tanzania Bara kwa ajili ya kuzitengeneza kuwa shule maalum za michezo na kwa kuanzia tunaanza na shule tisa kwa sasa. Hii itasaidia kuongeza miundombinu ya michezo mashuleni na tunashirikiana kwa ukaribu na Wizara ambayo ina dhamana ya Elimu na wenzetu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI katika kuhakikisha hili linatendeka.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili kwamba wakisawazisha uwanja kama tunaweza kuwapatia nyasi bandia. Kama nilivyojibu tatizo letu kubwa ni mipaka ya kibajeti ambayo tunayo lakini nitahakikisha nashirikiana na Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Vunjo kupata wadau kwa ajili ya kuwatafutia nyasi bandia wananchi hao kama watasawazisha uwanja wao, ahsante. Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha uwanja wa michezo katika eneo la Polisi Himo?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais alielekeza Serikali na Chama cha Mapinduzi mkae kwa ajili ya kurekebisa viwanja saba vya michezo; je, mmefikia hatua gani?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la nyongeza la Dkt. Kimei, viwanja hivi viko katika mipango yetu na sasa hivi tuko katika hatua ya kutafuta wakandarasi kwa ajili ya kukarabati viwanja hivi saba.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha uwanja wa michezo katika eneo la Polisi Himo?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ni kwa nini Wizara hii isishirikiane na TAMISEMI kuhakikisha inaboresha na kujenga miundombinu ya michezo kwenye shule zote za sekondari na msingi nchini kwa sababu kuna shule zingine hazina miundombinu hii?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu pia, mpango wetu ni kutengeneza viwanja vya michezo yote ya kipaumbele kwenye shule 56, shule mbili kwenye kila Mkoa wa Tanzania Bara kwa Mikoa 28 kwa sasa, kwa hiyo tunaendelea kushirikiana na wenzetu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kufanya jambo ambalo Mheshimiwa Mbunge analisema.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT.CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha uwanja wa michezo katika eneo la Polisi Himo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali kwa kuanza kufikiria kuuboresha Uwanja wa Jamhuri wa Morogoro kwa sababu ni uwanja wa Kimataifa na wanachezea michezo ya Kitaifa. Je, ni lini mtaanza kuuboresha uwanja huu? Ahsante.

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pindi rasilimali fedha itakapokuwa imekaa sawasawa kwenye Wizara yetu tutaanza kuukarabati Uwanja wa Jamhuri Morogoro.