Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 222 2024-02-15

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuunganisha reli ya TAZARA na Bandari ya Kasanga ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo katika ukanda huo hususani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa TAZARA inamilikiwa na Serikali mbili; Tanzania na Zambia, tumeanza mazungumzo na wenzetu Zambia ili kutenga fedha katika bajeti ya TAZARA kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa reli hiyo kwa lengo la kubaini gharama za ujenzi wake na manufaa yake kiuchumi.