Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT. S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya kutia matumaini kutoka Serikalini, naomba niulize maswali mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, juu ya efficiency ya TAZARA ni suala ambalo hatuna ubishani kama Taifa na hasa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, juu ya ufanyaji kazi bora wa TAZARA. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba ukarabati unafanyika na mtaji unawekwa ili TAZARA iweze kufanya kazi kwa jinsi ambavyo tunatarajia? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa na hivi tunavyoongea tayari imeshafanya upanuzi katika Bandari ya Kasanga, na lami imeshajengwa mpaka kufika Kasanga, je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka wa kuishirikisha sekta binafsi ili kuhakikisha kwamba kutoka Kasanga kwenda DRC na kui- decongest Bandari ya Dar es Salaam; na bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri anajua tuna makubaliano mazuri na DRC, ni wakati muafaka wa kufanya extension ili tuweze ku-decongest bandari yetu?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, TAZARA ni reli muhimu kwa uchumi wa Taifa letu. Sisi sote tunafahamu tangu ilipoanza kujengwa na kuanza kutumika mwaka 1976 kwa Sheria ya Bunge Na. 23 ya mwaka 1975 yenye urefu wa kilometa 1,860. Pia, sisi Watanzania tuna faida kubwa zaidi kwa sababu asilimia 52 ya reli hiyo ambayo ni 975 iko Tanzania na wenzetu ni 885.

Mheshimiwa Spika, ilipokuwa inatengenezwa wakati huo, ilikuwa imelenga kubeba mzigo wa tani milioni tano, lakini karibu miaka yote hiyo, hatukuwahi kufikia ufanisi huu, ni miaka michache tulifikia asilimia 24. Mamlaka za nchi kwa maana ya Tanzania, Zambia pamoja na wenzetu Wachina, baada ya kuitazama reli hii ndefu kabisa barani Afrika ambayo ina madaraja karibu 318, ina mahandaki karibia 22 na makaravati karibu 2,229, wakasema ipo haja ya kuanza kuitafakari upya.

Mheshimiwa Spika, hii inakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa tunaoufanya pale bandarini. Tayari Rais wetu na Marais hawa wawili wako kwenye mazungumzo. Tunategemea ukarabati mkubwa sana kwenye miundombinu pamoja na vitendea kazi unaweza ukaanza kufanywa mwaka huu 2024 ili kuiboresha bandari hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwenye hoja ya pili aliyoisema ya PPP, tunatambua ni hoja yake ya muda mrefu Mheshimiwa Mbunge, anajenga hoja kwamba kutoka Kaprimposhi mpaka kule Lubumbashi ni Kilometa 1,000 wakati kutoka kutoka pale Kasanga - Mlilo ukivuka ng’ambo ni kilometa 400.

Mheshimiwa Spika, tumepokea ushauri wake, tutaufikisha Serikalini ili tuuchakate kama tunavyochakata mambo mengine ili tuone namna gani tunakwenda kuutekeleza, ahsante.

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Supplementary Question 2

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Ni lini Serikali itajenga reli kutoka Bandari ya Mtwara kuja Tunduru – Namtumbo - Songea, pale Matomondo - Mbinga mpaka Mbamba Bay? Ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tayari tuko kwenye hatua ya kuhuisha design hiyo ya southern corridor kwa maana ya kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay mpaka Liganga na Mchuchuma. Itakapokuwa tayari, nafikiri Serikali itaanza kutekeleza mara moja.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupewa nafasi. Kwa kuwa kuna ushindani mkubwa wa Lobito Corridor, je, Serikali ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha miundombinu ya TAZARA inakuwa katika kiwango cha SGR?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, katika majibu ya nyongeza nimezungumza mpango wa Serikali wa kuiboresha vizuri sana TAZARA, ambapo tayari viongozi wetu wameshaanza mazungumzo na yatakapokuwa tayari tutaanza kuyatekeleza mwaka huu wa 2024.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Supplementary Question 4

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikiahidi ujenzi wa Reli kutoka Tanga – Arusha – Loliondo – Mugumu hadi Musoma, lakini ni miaka sasa imepita. Napenda kujua nini kauli ya Serikali kuhusiana na ujenzi wa hiyo reli?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer


NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge hoja hii aliyoizungumza ya Tanga – Arusha na Musoma baada ya hapa tupate muda wa kuijadili halafu tuweze kupata majibu kamili.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanza ujenzi wa kipande cha Reli ya TAZARA kutoka Tunduma hadi Bandari ya Kasanga?

Supplementary Question 5

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, inasemekana kwamba Kampuni inayomilikiwa na Serikali ya Uchina imeshatoa pendekezo la ukarabati wa reli husika kwa thamani ya shilingi trilioni 2.5 na majadiliano yalianza na Serikali ya Zambia kupitia Waziri mwenye dhamana kama wewe. Hiyo imekuwa reported na gazeti la Citizen la tarehe 10 Februari, 2024. Serikali mnatuambiaje kuhusiana na hili? Hayo unayoyasema ndiyo kampuni inayomilikiwa na Serikali ya China?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, mazungumzo yanaendelea na kwa kuwa hatujafika hatua ya mwisho, itakuwa ni mapema sana kuanza kuzungumzia gharama na hatua tuliyofikia. Namuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira, yakishakamilika taarifa hizi ni za wazi, basi ataweza kufahamu pengine ni mkandarasi gani anayefanya kazi hiyo.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu swali hili limekuwa likijirejea mara kwa mara na hili swali alilouliza Mheshimiwa Msongozi na umejibu hapa kwamba 2024 nafikiri ulikusudia kusema 2024/2025. Sasa ni muhimu ili 2024/2025 linahusu hii ya TAZARA au inahusu ile ya Mheshimiwa Jacqueline aliyouliza ile ya kuanzia Mtwara mpaka Mbamba Bay. Hii 2024/2025 inahusu ipi kati ya hizi mbili?

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, mwaka huu 2024 nilichokizungumzia ni uboreshaji wa Bandari ya TAZARA kutoka Dar es salaam mpaka Kapirimposhi kilomita 1860 hii Reli ya TAZARA kutoka Dar es salaam mpaka Kapirimposhi huu ndio uboreshaji tunaozungumza kwamba mazungumzo yanaendelea kati ya nchi hizi tatu na tunategemea mwaka huu pengine tuanze utekelezaji wake.

SPIKA: Sawa umerejea tena 2024, ukisema 2024 maana yake ni mwaka huu wa fedha ule unaokuja unaitwa 2024/2025 wewe unakusudia kusema upi 2023/2024 au 2024/2025?

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nilikusudia kusema kwa maana kuanzia Januari hii mpaka Desemba hapa katikati tutakuwa tumefikia hatua nzuri ya utekelezaji.