Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 28 2024-04-04

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali wa kulipatia Jimbo la Busanda Halmashauri, kwani michakato ya DCC na RCC iliwasilishwa TAMISEMI?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Geita iliwasilisha maombi ya kupandishwa hadhi Jimbo la Busanda kuwa halmashauri kwenda Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa barua ya tarehe 24 Machi, 2020. Maombi hayo yalifanyiwa kazi kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali imetoa kipaumbele katika kuboresha na kukamilisha miundombinu kwenye maeneo ya kiutawala yaliyopo ili yaweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baadaye kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa. Ahsante.