Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali wa kulipatia Jimbo la Busanda Halmashauri, kwani michakato ya DCC na RCC iliwasilishwa TAMISEMI?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Je, ni lini zoezi la uboreshaji maeneo yaliyopo litakamilika, ukizingatia jibu kama hili lilitolewa mwaka wa fedha uliopita?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Katika Jimbo la Busanda tuna Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro ambapo wakati tunapewa mamlaka mwaka 2014 kulikuwa na watu 86,231, lakini leo hii tunavyozungumza baada ya sensa, tuna watu 231,332 ikiwa ni ongezeko la watu 144,000. Tunakusanya mapato kama shilingi bilioni 1.3, tuna shule za msingi 24 na shule za sekondari 16. Je, nini mkakati wa Serikali kuipandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo ya Katoro kuwa Halmashauri ya Mji? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampa taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua sana umuhimu wa kuanzisha mamlaka mpya katika maeneo mbalimbali kote nchini ili kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi. Kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele kuboresha kwanza miundombinu, majengo ya Utawala, ofisi na majengo mengine ya huduma za kijamii katika mamlaka ambazo zipo ili ziweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baada ya kukamilisha zoezi hilo la kuwezesha miundombinu, tutakwenda kuanzisha mamlaka nyingine. Kwa hiyo, tamko la Serikali litatolewa muda ukifika kwa ajili ya kazi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusiana na kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Katoro ambayo ni mamlaka ya mji, hili nalo linaenda sambamba na jibu langu la msingi kwamba baada ya kukamilisha taratibu hizo, basi tutaona namna ya kufanya kama itakidhi vigezo. Ahsante.