Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 29 2024-04-04

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itawalipa posho Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji na kuongeza posho ya Madiwani ili kuwasaidia kutekeleza majukumu yao kikamilifu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi. Serikali imeendelea kulipa posho za Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni 1.7 ambapo kufikia Februari, 2024 shilingi bilioni 1.15 zimetolewa kwa ajili ya kulipa posho za Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetenga shilingi bilioni 20.8 kwa ajili ya kulipa posho za Waheshimiwa Madiwani katika halmashauri 168 ambapo kufikia Februari, 2024 kiasi cha shilingi bilioni 13.5 kimetolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuongeza na kuboresha vyanzo vyake vya mapato ili kuendelea kulipa posho za Waheshimiwa Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa kwa ufanisi zaidi. Ahsante.