Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itawalipa posho Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji na kuongeza posho ya Madiwani ili kuwasaidia kutekeleza majukumu yao kikamilifu?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, naleta swali hili kwa mara ya sita, lakini nataka kumpa taarifa Mheshimiwa Naibu Waziri ajue Mbulu Vijijini, Wenyeviti wa Vitongoji hawajawahi kupata hizi posho. Je, lini wanapata posho hizi ili kukidhi na kuweza kufanya shughuli zao kama swali langu linavyosema?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Niliwauliza, lini mnawaongezea posho Waheshimiwa Madiwani? Sikuuliza kama mnaendelea kuwalipa, nimeuliza, “lini”? Naomba jibu, lini mnawaongezea posho Waheshimiwa Madiwani ili waweze kufanya kazi kama inavyostahili? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nampongeza Mheshimiwa Flatei Massay, ni kweli ameuliza swali hili mara kadhaa kwa nia njema ya kutaka kuona Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa wanapata posho zao za kila mwezi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inathamini sana kazi za viongozi hao. Ndiyo maana imeendelea kutenga fedha kupitia Serikali Kuu na mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya kulipa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vitongoji vya halmashauri hiyo ambavyo havijalipwa, nimwelekeze Mkurugenzi wa Mbulu Vijijini kuanza kutenga fedha kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza kulipa posho kwa kadri ya maelekezo ya Sheria na Miongozo iliyopo ili viongozi hao wapate posho zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuhusu hoja ya lini tunapandisha posho za Waheshimiwa Madiwani, Serikali inaendelea kufanya tathmini ya kuona uwezo wake wa kifedha na baadaye itatoa tamko kuhusu namna gani tunakwenda kulifanyia kazi suala hilo. Ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itawalipa posho Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji na kuongeza posho ya Madiwani ili kuwasaidia kutekeleza majukumu yao kikamilifu?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa Serikali inatenga fedha nyingi kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kwa sababu tunajua umuhimu wa wenyeviti hawa, ni lini tutaona umuhimu wao kwa kuwalipa posho isiwe fedha kama sasa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba posho za viongozi hao ambao ni Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa siyo fedha. Zipo kwa mujibu wa Mwongozo na Serikali inahakikisha inalipa wenyeviti hao kwa kadri fedha zinavyopatikana. Changamoto iliyopo ni uwezo wa halmashauri zetu kulipa wenyeviti wote kwa wakati, ndiyo maana Serikali inaendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuwezesha halmashauri kukusanya zaidi ili ziweze kulipa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuwasisitiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini kuongeza uwezo wa halmashauri na kuweka kipaumbele katika kuwalipa viongozi hao. Ahsante.