Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 30 2024-04-04

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kumaliza tatizo la uhaba wa Walimu Shule za Sekondari na za Msingi katika Wilaya ya Ikungi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Hanje, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha miaka mitatu 2021 hadi 2023, Serikali iliajiri jumla ya walimu wa shule za sekondari 13,128 na walimu 16,751 wa shule za msingi na kuwapangia vituo kote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi hicho cha miaka mitatu, 2021 hadi 2023 Serikali imeajiri na kuwapanga jumla ya walimu 314 katika Halmashauri ya Ikungi. Kati yao, walimu 240 ni wa shule za msingi na walimu 74 ni wa shule za Sekondari.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuajiri walimu na kuwapangia vituo mara baada taratibu za kibali kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kukamilika kwa ajili ya kuongeza walimu katika maeneo yenye uhitaji mkubwa.