Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 31 2024-04-04

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaweka pipes za gesi Jijini Dar es Salaam kila nyumba ili wananchi wapikie nishati nafuu?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Jimbo la Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imeshasambaza miundombinu ya gesi asilia katika nyumba 880 katika Jiji la Dar es Salaam. Pia imejenga bomba la gesi (pipe) lenye urefu wa kilomita 12.4 kutoka Mwenge hadi Mbezi Beach kupitia barabara ya Bagamoyo na tayari viwanda viwili na hoteli sita zimeshaunganishwa na bomba hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha wananchi wengi Jijini Dar es Salaam wanatumia gesi asilia, TPDC kwa kushirikiana na Kampuni ya TAQA Dalbit inafanya utafiti za mahitaji ya gesi asilia kwa njia za kusambazia utakaokamilika Julai, 2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, utafiti huu utaonesha namna bora ya kufikisha mabomba kwenye maeneo yenye changamoto na utabainisha maeneo gani yanayoweza kupelekewa mabomba na maeneo gani hayawezi kupelekewa mabomba ambapo njia nyingine zitatumika kuhakikisha gesi inawafikia wananchi. Ahsante