Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka pipes za gesi Jijini Dar es Salaam kila nyumba ili wananchi wapikie nishati nafuu?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa mkakati wake wa kuhakikisha kwamba sasa tunakwenda kupata nishati safi na salama ya kupikia. Ni jambo kubwa, tunampongeza sana na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wamelipokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wamehamasika na wako tayari katika matumizi ya nishati safi ya gesi ya kupikia, lakini kwa kuwa changamoto kubwa ni gharama ya hiyo gesi na Serikali imeonesha mipango ya kusambaza gesi hiyo ambayo ina gharama nafuu kwa wananchi, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuelekeza nishati hiyo au mabomba hayo kwenye maeneo yenye wananchi wengi kama Kawe, Mwenge, Mbagala, Manzese na maeneo mengine, badala ya ku-base kwenye eneo hilo hilo la Mbezi Beach na Mikocheni peke yake?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tunao mpango wa kuhamasisha matumizi ya gesi asilia nchini, na kwa sasa hivi tunao mkakati wa kupeleka gesi kwenye nyumba takribani 10,000. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo hayo ambayo ameyataja yenye watu wengi yatafikiwa na huduma hii ili waweze kutumia gesi kwa gharama nafuu zaidi kwa sababu gesi hii inayounganishwa majumbani ina unafuu zaidi kuliko gesi ile ya LPG ya mitungi. Ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka pipes za gesi Jijini Dar es Salaam kila nyumba ili wananchi wapikie nishati nafuu?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Serikali imehamasisha matumizi ya nishati safi na Watanzania wengi hasa wa vijijini wamehamasika, lakini bei, kwa maana ya gharama ya ujazaji wa gesi ni kubwa sana. Nataka kujua, nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha inatoa ruzuku ili kupunguza gharama za gesi kusudi wale wananchi maskini wa kijijini waache kutumia kuni na mkaa, watumie gesi?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunao mkakati wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ambao tunaenda kuukamilisha hivi karibuni ili kuweka mkakati wa kukabiliana na changamoto zote ambazo zinawazuia wananchi wasiweze kutumia gesi katika kupikia. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, baada ya mkakati huu kukamilika, tutakuwa na mikakati madhubuti wa kuwawezesha wananchi wote kutumia gesi safi ya kupikia ili kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.