Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 32 2024-04-04

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kupeleka walimu katika Chuo cha VETA Kitangari ili kuleta ufanisi wa elimu inayotolewa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kupeleka Walimu katika Chuo cha VETA cha Kitangari kwa ajili ya kuleta ufanisi na tija katika elimu na mafunzo ya ufundi stadi yanayotolewa kwa wananchi wa Newala ili waweze kushiriki vema katika kutekeleza shughuli zao za kiuchumi na kuchangia pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeshapeleka jumla ya walimu sita katika Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Newala kilichopo Kitangari ili kuwezesha utoaji wa mafunzo katika fani tatu zilizopo pamoja na masomo mtambuka. Aidha, katika ikama na bajeti ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imekasimia walimu watatu wa masomo mtambuka ambayo utekelezaji wake utafanyika baada ya kuidhinishwa utekelezaji wa ikama hiyo. Nakushukuru.