Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kupeleka walimu katika Chuo cha VETA Kitangari ili kuleta ufanisi wa elimu inayotolewa?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, napenda kufahamu mkakati ambao Serikali inao katika kuajiri watumishi ambao sio walimu. Kwa mfano, pale chuoni hakuna matron, hakuna patron, hakuna dereva wala wapishi, mkakati ukoje ili huduma ziweze kutolewa kwa ukamilifu katika chuo kile?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Kupitia majibu ambayo Serikali imeyatoa, imeonesha kwamba fani ziko tatu, na ni kweli fani tatu tu ambazo zinatolewa kati ya fani nyingi ambazo tunatarajia zitolewe ili wanafunzi wengi au wananchi wengi wapate nafasi ya kupata ujuzi. Mfano, hakuna fani ya mafundi magari, hatuna fani ya ujenzi, hatuna fani ya uunganishaji wa vyuma pamoja na mabomba. Mpango wa Serikali wa kuongeza fani nyingine ukoje ili kuwakwamua wananchi wa Newala ambao wanahitaji fani hizi ili waweze kujiendeleza kimaisha? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna kuhusiana na suala la watumishi wasiokuwa walimu, naomba nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Maimuna kwamba kunapo mwezi wa Tatu mwaka huu, 2024 tayari tulishatangaza nafasi za watumishi wasiokuwa walimu kwa vyuo vyetu vyote vya VETA. Kwa hiyo, mara tu baada ya mchakato huu kukamilika, baadhi ya watumishi watakaopatikana tutawapeleka katika chuo hiki cha Kitangari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kuhusiana na suala la kuongeza fani, Mheshimiwa Maimuna nadhani anafahamu kuna maboresho ambayo tunaendelea pale kwa maana ya ujenzi wa mabweni na ukarabati wa karakana pamoja na madarasa. Kwa hiyo, tutaendelea kuboresha kwanza miundombinu na baada ya uboreshaji huo wa miundombinu, utaratibu wa kuongeza fani sasa tutaweza kuufanya ili uweze kuendana na miundombinu iliyopo katika eneo hilo. Ahsante.