Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 33 2024-04-04

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, masuala ya “kwa niaba, na jina la Mbunge” yameshatolewa. Kwa hiyo, nenda moja kwa moja kwenye jibu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunikumbusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea na jitihada za kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili liweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limepata jumla ya magari 12 ya Zimamoto na Uokoaji yaliyopatikana kutoka katika mkopo wa Euro milioni 4.9 kutoka katika Serikali ya Austria ambapo yatasambazwa katika vituo vilivyoainishwa, kikiwemo Kituo cha Temeke. Vituo vingine vitakavyonufaika ni pamoja na Ilala, Kinondoni, Dodoma, Mwanza, Morogoro, Mbeya, Arusha na Kilimanjaro.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha taratibu zote za mkopo wenye masharti nafuu wa thamani ya Dola za Marekani milioni 100 kutoka Taasisi ya ADEX iliyopo Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa ajili ya kupata vitendea kazi mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa magari 150 ya zimamoto na uokoaji kwa matumizi ya nchi nzima. (Makofi)