Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Hata hivyo, mara nyingi magari haya yanapokwenda kuzima moto, maji yanaisha katikati. Je, Serikali ina mkakati gani wa kununua maboza ya maji ambayo yataweza yakavutwa pale maji yanapokwisha kwenye magari ya kuzimia moto ili kutumika kuzima moto? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali itagawa lini magari haya ambayo ameyasema katika vituo mbalimbali ambavyo amevitaja vikiwemo Temeke, Ilala na Mikoa mingine? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika magari yaliyowasili pale Dar es Salaam tunayo magari maalum ya maboza ambayo kazi yake kubwa ni kubeba maji ya msaada pale ambapo yale magari ya oparesheni yanapoishiwa. Magari yale yana uwezo wa kubeba maji kuanzia lita 5,000 mpaka 10,000. Katika mazingira ya kawaida, mazingira yale yatasaidia sana katika kuboresha huduma za kuzima moto kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya swali lake la pili ambalo…
MHE. DOROTHY G. KILAVE: (Hapa hakutumia kipaza sauti)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Naam!

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mtayagawa lini hayo magari ambayo tayari yapo? (Kicheko)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, yale magari yanasubiri tu utaratibu wa kuzinduliwa na baada ya uzinduzi wake, magari yale yataenda kwenye operesheni mara moja. Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, je, kutokana na ongezeko kubwa la watu katika Jimbo la Mbagala, Serikali haioni ipo haja ya kuanzisha Kituo cha Uokoaji na Zimamoto katika Jimbo hilo? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Chaurembo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tumezingatia hilo na ndiyo maana unaona katika mpango unaokuja, tunaleta magari karibu 100 yatakayogawiwa nchi nzima na Mbagala tutaiangalia kwa upekee wake. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Miji wa Liwale ni Mji unaokua kwa haraka sana. Sasa tunahitaji kuwa na Kituo cha Zimamoto pamoja na vifaa. Ni lini Serikali itatuletea vifaa vya zimamoto kwenye Wilaya ya Liwale?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia swali dogo la Mheshimiwa Kuchauka, katika mpango unaokuja wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ni kuhakikisha huduma hizi za zimamoto zinaimarishwa nchi nzima. Hivyo, tumechukua ombi lake na tutapita huko na kuangalia vile vigezo vinavyostahili kuanzisha Kituo cha Zimamoto katika Wilaya yake. Ahsante. (Makofi

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Waziri amesema kwamba kuna magari ambayo yatanunuliwa, katika Manispaa ya Shinyanga hatuna gari la zimamoto, tunatumia magari ya wadau. Je, Shinyanga itakuwa katika mgao huo? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kwamba katika yale magari yatakayokuja awamu ya pili ambayo ni magari zaidi ya 100, yanalenga kuhudumia mikoa yote ya Tanzania na katika mazingira ya kawaida, Shinyanga itakuwemo.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kununua Magari ya Zimamoto kwa ajili ya Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Mchicha – Temeke?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mkoa wetu wa Iringa, tunayo misitu katika Wilaya ya Mufindi na Kilolo na kumekuwa kuna na mioto inayojitokeza kila wakati. Tunaiomba Serikali iangalie katika huo mgao, basi isikose katika Mkoa wetu wa Iringa kutupatia gari la zimamoto. Ahsante. (Makofi

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ombi la Mheshimiwa Mbunge limepokelewa na litafanyiwa kazi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hii siyo Wizara ya Mheshimiwa Waziri Pinda, lakini amejibu kama mwendokasi. Ahsante sana. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)