Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 34 2024-04-04

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:-

Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara kwa utaratibu wa EPC+F unahusisha kufanya usanifu wa barabara kabla ya kuanza ujenzi. Kwa sasa Mkandarasi ameanza na anaendelea na usanifu wa kina. Aidha, Serikali na wakandarasi wanaendelea na taratibu za kupata fedha kwa ajili ya malipo ya awali kwa miradi yote ya EPC+F ukiwemo huu wa barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo hadi Lumecha Mkoani Ruvuma. Ahsante.