Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini kwa sasa wakati tunasubiri mchakato huo, barabara ya Malinyi imefungwa, haipitiki kwa maana ya barabara ya TANROADS. Je, Serikali ipo tayari kupeleka fedha za dharura kwa Meneja wa TANROADS wa Mkoa kwa ajili ya kutatua dharura hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba TANROADS tayari wanaendelea na shughuli za kuifungua barabara. Tulituma fedha za awali, na tayari Meneja wa Mkoa wa Morogoro, mkoa ambao umeathirika sana, ameishaingiziwa fedha tangu jana kwa ajili ya kuendelea kufungua barabara ambazo zimejifunga. Ahsante. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mlowo – Chitete – Kamsamba ilitengewa bajeti mwaka huu wa fedha 2023/2024 na sasa hivi tumebakiwa na miezi miwili tu. Swali langu kwa Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba, tutarajie kuna pesa yoyote atatupelekea kuanza kujenga kilomita zozote au ndiyo tunyamaze hivyo hivyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Mlowo – Kamsamba tayari imeshapata kibali, itatangazwa muda siyo mrefu ili tuanze kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa taratibu zote zimeshakamilika kwa hiyo barabara ya Mlowo – Kamsamba, nilitaka kujua sasa, lini itatangazwa rasmi ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyomjibu Mheshimiwa Condester Sichalwe, ndiyo barabara hiyo hiyo kwamba tutaitangaza muda wowote ili ianze kujengwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 4

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Masasi – Nachingwea ilisainiwa mkataba kwa utaratibu wa EPC+F, ni lini itaanza kujengwa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi la swali hili, barabara zote za EPC+F tunategemea zilishasainiwa na tumesema kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha itakuwa tayari wakandarasi wameshaanza kwenda site kwa ajili ya kuanza kuzijenga. Ahsante. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 5

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 20 Machi, Makamu wa Rais alifanya ziara Jimbo la Hai na aliagiza kutekelezwa kwa ahadi za Mheshimiwa Rais za Ujenzi wa barabara ya Kwasadala – Kware – Remira, Kwasadala - Bwani na Bomang’ombe - TPC. Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hizi utaanza? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelekezo ya Mheshimiwa Makamu wa Rais, barabara hii tutaiingiza kwenye bajeti kwa sababu zilikuwa zinafanyiwa usanifu, zianze kufanyiwa usanifu ikiwa ni maandalizi ya kuzijenga hizo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Usa River kwenda mpaka Oldonyosambu ujenzi wake ulisimama kwa muda mrefu baada ya kufika lango la ANAPA. Je, ni lini Serikali itaendelea na ujenzi huo kutoka Ngarenanyuki hadi Oldonyosambu? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusaidiana na wenzetu wa TAMISEMI, barabara hii ni kweli ilisimama, lakini tunaendelea kutafuta fedha ili mvua itakapokatika, basi tuendeleze kuijenga hiyo barabara. Ahsante.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 7

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Kilolo kupitia Kidabaga kwenda Idete hadi sasa haipitiki kutokana na maporomoko. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za dharura kwa ajili ya kuifanya ile barabara iweze kupitika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer


NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge alifika ofisini na tayari Mheshimiwa Rais ameshatoa fedha za dharura. Kwa hiyo, Meneja wa Mkoa wa Iringa ameshapewa maelekezo aende akafungue hiyo barabara ambayo imejifunga. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Mkandarasi wa Barabara ya Lupilo, Malinyi, Kilosa kwa Mpepo hadi Londo ataanza kazi kwa mtindo wa EPC + F?

Supplementary Question 8

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna barabara ile ya Mtwara – Pachani ambayo inakwenda mpaka Nalasi upande wa Tunduru, ni barabara ya kiulinzi pia. Je, ni lini hasa Serikali itaanza kuijenga barabara ile kwa lami kama ilivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi 2025? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja yenye urefu wa kilomita 300, Serikali inachofanya sasa hivi ni kuhakikisha kwamba inapeleka fedha kwa ajili ya kuijenga kwa lami ama kwa zege na kutengeneza madaraja ili iweze kupitika kwa mwaka wote wakati Serikali inafuta fedha ya kujenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.