Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 35 2024-04-04

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. SEIF K. GULAMALI aliuliza:-

Je, ni adhabu gani inatolewa kwa Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wanaobainika kudhuru raia na mali zao?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Misitu Sura 323 imeweka makatazo ambayo mtu yeyote anayekiuka makatazo hayo anakuwa ametenda makosa ya jinai na hivyo kulazimika kuchukuliwa hatua za kisheria. Aidha, katika utekelezaji wa majukumu hayo, watumishi wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni na misingi ya haki za binadamu. Hivyo, endapo mtumishi atabainika kudhuru raia au mali zake, atakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma za mwaka 2022 na kanuni zake pamoja na Amri za Kudumu za Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu za Mwaka 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo mtumishi wa TFS atabainika kukiuka masharti ya kazi na kama atakuwa ametenda kosa la kijinai na kinidhamu, mwajiri atamfungulia mashtaka kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma zikisomwa pamoja na kifungu cha 9(3) cha Amri za Jeshi la Uhifadhi za Mwaka 2022. Pindi mtumishi huyo akikutwa na hatia, anaweza kufukuzwa kazi, kupunguziwa mshahara au kushushwa cheo na mshahara.