Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. SEIF K. GULAMALI aliuliza:- Je, ni adhabu gani inatolewa kwa Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wanaobainika kudhuru raia na mali zao?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia kutokana na madhara wanayopata raia kwa vitendo vya baadhi ya watumishi wabaya wa TFS? Ahsante.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almasi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, masuala yote ya haki za binadamu yanatekelezwa kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo. Nimhakikishie Mheshimiwa Almasi, pale watumishi wetu watakapokuwa wamefanya makosa chini ya sheria hizo, fidia stahiki zitatolewa kwa mujibu wa sheria iliyopo. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. SEIF K. GULAMALI aliuliza:- Je, ni adhabu gani inatolewa kwa Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wanaobainika kudhuru raia na mali zao?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itawalipa fidia kwa kifuta machozi kwenye Vijiji vya Hunyari, Kihumbu, Mariwanda, Sarakwa, Mugeta Kyandege na Tingirima?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kufanya uhakiki na uthamini wa madai ambayo tumeyapokea na pindi uthamini huo utakapokamilika, tutawalipa wahusika haraka iwezekanavyo.