Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 37 2024-04-04

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanzisha Kituo cha Madume Bora ya Ng’ombe Wilayani Bahi?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea na utekelezaji wa Mpango wa Mabadiliko ya Sekta ya Mifugo wa Miaka Mitano Kuanzia Mwaka 2022/2023 hadi Mwaka 2026/2027. Aidha, kupitia mpango huo, uboreshaji wa mbari za ng’ombe unafanyika kupitia matumizi ya madume bora na uhimilishaji ambapo kwa upande wa madume, Wizara imesambaza bure madume bora ya ng’ombe wa nyama 366 kwenye vikundi vya wafugaji katika halmashauri nane ili kuzalisha mifugo yenye tija zaidi ile ya asili.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Wizara kwa sasa ni kusambaza madume bora ya ng’ombe kwa vikundi vya wafugaji ili kuboresha mifugo yao badala ya kuanzisha vituo vya madume. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Wizara imepanga kununua madume bora 200 yatakayosambazwa kwa vikundi vya wafugaji, wakiwemo wafugaji wa Halmashauri ya Bahi ambao watapewa madume 20. Naomba kuwasilisha.