Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 118 2024-04-19

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:-

Je, lini barabara za lami zinazofadhiliwa na Benki ya Dunia zitaanza kujengwa Mbogwe?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Mradi wa RISE katika Wilaya ya Mbogwe zina jumla ya urefu wa kilometa 102. Barabara zitakazojengwa kwenye Mradi huo ni Masumbwe – Iponya - Nyashimba (kilometa 20), Lulembela – Kiseke – Isebya (kilometa 17), Mkweni – Nhomolwa - Nyanhwiga (kilometa 21), Ishigamva – Busabaga – Ilolangulu (kilometa 14) na Ivumwa – Ushirika - Shibutwe (kilometa 30).

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu utafanyika kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa Barabara za Masumbwe – Iponya – Nyashimba (kilometa 20), Lulembela – Kiseke – Isebya (kilometa 17), Ishigamva – Busabaga – Ilolangulu (kilometa 14) na Mkweni – Nhomolwa – Nyanhwiga (kilometa 21). Aidha, kazi za usanifu wa barabara za awamu ya kwanza zilianza Januari, 2024 na zinatarajiwa kukamilika Agosti, 2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kazi ya usanifu wa barabara kukamilika Serikali kupitia TARURA itatangaza zabuni na kumpata mkandarasi wa kujenga barabara za awamu ya kwanza kwa kiwango cha lami.