Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:- Je, lini barabara za lami zinazofadhiliwa na Benki ya Dunia zitaanza kujengwa Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali la kwanza; kwenye Wilaya ya Mbogwe kuna hizo barabara alizozitaja Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna madaraja ambayo hayapitiki kabisa sasa hivi pamoja na kwamba nashukuru kwa majibu ya Serikali. Je, Serikali ina mpango gani wa kulitengeneza na Daraja la Ikalanga – Ilangale kwa sababu sasa hivi haipitiki na wakulima wamelima mazao mengi ambayo yanatarajiwa kutoka huko?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; mpango wa Serikali wa kuunganisha kwa kiwango cha lami wilaya na mkoa. Je, ni lini sasa Serikali itaitimiza ahadi hii ili kuunganisha Wilaya ya Mbogwe na Geita kwa kiwango cha lami?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza Mheshimiwa Mbunge, naomba nitumie nafasi hii kumwagiza Meneja wa TARURA katika Wilaya ya Mbogwe ili aweze kwenda kufanya tathmini na kubaini kwamba barabara hiyo inahitaji kupatiwa fedha za dharura kwa ajili ya kuirekebisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la kuunganisha wilaya na mkoa, tutaendelea kufanya tathmini na kuzingatia uhitaji na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi.