Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 121 2024-04-19

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanzisha utekelezaji wa mpango wake wa kuanzisha vituo maalum vya masuala ya uwekezaji na masoko kwa wanawake kila kata?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya EPZA imetenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha kanda maalum za kiuchumi katika mikoa mbalimbali nchini. Lengo kuu la kuanzisha maeneo haya ni kuhamasisha uwekezaji wa viwanda vya kuongeza thamani mazao mbalimbali yanayozalishwa nchini na kukuza mauzo ya nje ya bidhaa za viwandani na pia kuzalisha bidhaa zinazoagizwa nje kwa soko la ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuendeleza maeneo haya kuna sehemu zitatengwa kwa ajili ya wajasiriamali wadogo na wa kati (SME’s) wakiwemo wanawake na vijana ili waweze kuanzisha viwanda vya kuchakata na kutengeneza bidhaa mbalimbali kwa ajili ya soko la ndani na nje. Aidha, maeneo haya yatatumika kama incubators kwa maana ya atamizi ili kukuza wajasiriamali wadogo. Nakushukuru.