Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanzisha utekelezaji wa mpango wake wa kuanzisha vituo maalum vya masuala ya uwekezaji na masoko kwa wanawake kila kata?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali haioni umuhimu wa kuwasaidia wanawake wajasiriamali wanaofanya biashara pembezoni mwa barabara hususan wale wanaokuwa na watoto wadogo kwa kuwatafutia maeneo ya muda wa kati wanasubiri kuwatengea maeneo husika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, ni lini sasa kituo cha uwekezaji kitaona umuhimu wa kuwasaidia kutengeneza program ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali wadogo hususan wanufaika wa mikopo ya Serikali ili fedha zile ziweze kurudi kwa kuwekezwa sehemu sahihi na kuwaonesha fursa zinazowazunguka katika maeneo yao?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna changamoto kubwa ya maeneo ya ufanyaji biashara hasa kwa akinamama wajasiriamali wadogo na vijana ambao wanauza biashara ndogondogo na wengi wanatumia maeneo ya barabarani au kando ya barabara kuuza bidhaa zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaanza kutenga maeneo kwenye halmashauri na miji ambako tunahamasisha hawa akinamama na wengine ambao hawana maeneo maalum ili waweze kufanya biashara zao katika maeneo hayo ambayo ni salama na sahihi kulingana na ubora hasa kwenye vyakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, kituo chetu cha uwekezaji kimekuwa kikitoa vivutio maalum kwa Watanzania na hasa kikilenga wajasiriamali au wafanyabiashara wanawake na vijana. Ndiyo maana kupitia program hii ya kuwezesha akinamama na vijana, Mheshimiwa Rais ameanza kuja na mpango maalum ambao kupitia mikopo hii ya 10% itakuwa ni sehemu ya kichocheo cha kuwasaidia akinamama hao ili wapate fursa za kuwekeza na kukua zaidi katika biashara zao. Nakushukuru.