Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 122 2024-04-19

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-

Je, kuna fursa na changamoto gani kwa Tanzania kushiriki kwenye biashara ya carbon.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna fursa kubwa ambayo Tanzania inanufaika katika biashara ya kaboni. Fursa ya kwanza ni uhifadhi wa baioanuai na pili, ongezeko la pato la Taifa. Hivi karibuni halmashauri mbalimbali zimepokea fedha zilizotokana na biashara ya carbon kutoka katika kampuni mbalimbali ambazo zinatumika kujenga miundombinu ya kusaidia jamii katika halmashauri mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na fursa zilizopo bado kumekuwa na changamoto kadhaa katika biashara ya kaboni. Kwanza ni uelewa mdogo wa jamii katika utekelezaji wa biashara ya kabon na pili ni uwazi wa biashara ya kaboni katika soko la dunia. Pamoja na changamoto hizo, Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wadau wote ili kuhamasisha uwekezaji wa miradi ya biashara ya kaboni katika sekta mbalimbali pamoja na biashara ya kaboni kwa wadau mbalimbali ili kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu biashara hii, ahsante.