Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 123 2024-04-19

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaenzi na kuwatunza Waasisi wa Muungano?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman Haroub Suleiman, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetunga Sheria maalum Na. 18 ya Mwaka 2004 mahususi kwa ajili ya waasisi hao wa Muungano wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pamoja na sheria hiyo imetungwa kanuni ya mwaka 2005 inayoweka utaratibu wa namna ya kuwezesha waasisi wetu, ikiwemo kuhifadhi kumbukumbu zao, kazi zao na kueneza falsafa zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Idara Maalum ya Kuwaenzi Waasisi imeundwa ikiwa chini ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka ya Taifa, ikishughulikia na kusimamia ukusanyaji na uhifadhi wa kumbukumbu na vitu vya waasisi wa Taifa kwenye umuhimu wa kihistoria. Aidha, Serikali inaendelea kuhakikisha kuwa kila mwaka kumbukumbu za kifo cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume pamoja na maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zinafanyika, ahsante.