Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaenzi na kuwatunza Waasisi wa Muungano?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kuna baadhi ya viongozi ambao walitumikia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwemo Dkt. Salmini Amour Bin Jumaa, anaishi kwenye hali ngumu sasa hivi kwa maana kwamba nyumba yake inaendelea sasa hivi kupata erosion, ipo karibu na bahari. Je, Serikali ama Ofisi hii ipo tayari kushirikiana na Kamati ya Viongozi Wakuu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ili kutatua changamoto hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji kutunzwa, lakini mpaka hivi sasa maeneo hayo yanakuwa kwenye hali hatarishi ikiwemo shule aliyosoma Mzee Karume. Je, Serikali ina mpango gani kutunza maeneo kama hayo? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Haroub. Naomba niseme Mheshimiwa Haroub ni mfuatiliaji sana na watu kule Baraza la Wawakilishi lazima wajue recognition yake ya kazi kubwa anayofanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, tulikuwa na sheria yetu ambayo nimezungumza hapa, lakini hii ilikuwa inagusa maeneo mahususi, kwa sababu mimi ni Waziri wa Muungano haya mambo ambayo amezungumza, mengine tutayachukua kwa ajili ya kuyafanyia kazi kupitia taratibu zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mambo ya kumbukumbu ya maeneo hayo niseme, kwa sababu ofisi yangu inahusika na mambo mbalimbali na kwa sababu ofisi yangu inashirikiana vizuri na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, kule Zanzibar, tunalichukua jambo hili, tunali-discuss halafu tuone way forward, tunafanyaje kuboresha maeneo hayo. (Makofi)