Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 125 2024-04-19

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MH. ALLY J. MAKOA aliuliza:-

Je, lini umeme wa REA utapelekwa Mitaa ya Chemchem, Tampori, Kwamtwara, Guluma, Mongoroma, Chandimo, Chang’ombe na Tura?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imeendelea kutekeleza kazi ya kusambaza umeme katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mitaa ambayo ipo katika mamlaka za miji na miji midogo yenye hadhi sawa na vijiji. Kwa kuwa Jimbo la Kondoa Mjini lipo katika mamlaka ya mji, kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024, REA itapeleka umeme katika mitaa 15 ambayo imefikiwa na miundombinu ya msongo wa kati, ikiwemo Mitaa ya Chemchem, Tumbelo na Chang’ombe. Aidha Mitaa ya Tura na Tumbelo imepatiwa umeme kupitia Mradi wa Ujazilizi Mbili (A). Serikali kupitia REA itaendelea kuratibu kazi ya kusambaza umeme katika vitongoji na mitaa ambayo haina umeme kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.