Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 129 2024-04-19

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuepuka mzigo mkubwa wa ulipaji wa fidia wakati inapoongeza ukubwa wa barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007, iliongeza upana wa hifadhi ya barabara kutoka meta 45 hadi meta 60 kwa barabara kuu na za Mikoa ili kukidhi mahitaji ya uendeshaji wa miundombinu ya barabara kwa wakati huu na wakati wa baadaye, ili uendane na ongezeko la watu na ukuaji wa shughuli za kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kupunguza ulipaji wa fidia Wizara, kupitia TANROADS, imefanya tathmini ya awali ya gharama inayohitajika kwa ajili ya kulipa fidia kwa mali zilizomo ndani ya eneo la hifadhi ya barabara lililoongezeka la meta 7.5 kila upande na kuonesha kuwa, gharama kubwa za fidia ziko katika majiji na miji. Kutokana na hali hiyo, Serikali inaangalia uwezekano wa kuchepusha barabara kwenye maeneo hayo. Aidha, uchambuzi wa kina unafanyika, ili kubaini ni barabara zipi kweli zinahitaji upana wa eneo la hifadhi ya barabara wa meta 60 kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na ya hapo baadaye ya kuzipanua kulingana na ongezeko la wingi wa magari. Zoezi hili likikamilika taarifa kamili itatolewa, ahsante. (Makofi)