Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuepuka mzigo mkubwa wa ulipaji wa fidia wakati inapoongeza ukubwa wa barabara?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kule Jimboni Kibaha kuna kipande cha Mlandizi kwenda Station ya SGR, Ruvu na Kongowe Soga, ambacho kinaunganisha na reli ya mwendokasi ambayo inatarajiwa kuanza kufanya kazi. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kujenga barabara hizi kwa haraka ili ziweze kutoa huduma kwenye hizo station za abiria?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; wananchi wa Majimbo manne ya Bagamoyo, Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Kisarawe walikuwa wanapata majibu tofauti kila wanapouliza swali lao linalohusiana na Barabara ya Makofia –Mlandazi – Mzenga hadi Vikumburu. Sasa kwa kuwa, majibu ya Serikali ni tofauti mara kwa mara, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kwenye kipindi hiki cha Bunge kutenga muda kuambatana na Waheshimiwa Wabunge wa maeneo hayo kwenda kutoa msimamo wa Serikali juu ya utaratibu wa ujenzi wa barabara hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kipande cha barabara cha Mlandizi kwenda Ruvu Junction ambacho kina kilometa 23, ni kati ya zile barabara ambazo wakati SGR inajengwa zinatakiwa ziunganishwe na miji ama vijiji ama centers ambazo zipo karibu na reli kwa ajili ya kuunganisha na hii ni barabara mojawapo. Kwa kuwa, barabara hii inahusisha barabara illiyokuwa ya TANROADS na TARURA kuna maeneo ambayo yalikuwa hayajasanifiwa. Kwa hiyo, ili kuharakisha ujenzi wa barabara hii, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Kibaha kwamba, tumeamua kutumia utaratibu wa design and build yaani unasanifu, Mkandarasi atasanifu na kujenga. Hivi tunavyoongea, tayari tuko kwenye hatua za mwisho za kumpata mkandarasi kwa ajili ya kujenga kilometa zote 23 kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Makofia – Mlandizi – Maneromango kwenda Vikumburu, tathmini imeshafanyika ya fidia. Najua Mheshimiwa Mbunge anataka kujua wananchi wanataka kujua italipwaje? Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tukubaliane ni lini tutapata nafasi, ili twende tukaongee na wananchi hao kuwaeleza mpango wa Serikali kuhusu barabara na fidia ambayo wanadai, ahsante. (Makofi)