Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 136 2024-04-22

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaupatia Mji wa Kibaha hadhi ya Manispaa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, halmashauri huanzishwa au kupandishwa hadhi kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Sura ya 287 na 288 pamoja na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa mwaka 2014.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilipokea wasilisho la Halmashauri ya Mji wa Kibaha kwa mara ya kwanza mwaka 2016 na kuchambua kwa kuzingatia vigezo ambapo haikukidhi vigezo. Maelekezo yalitolewa kwa ajili ya maboresho. Uchambuzi wa awamu ya pili ulifanyika mwezi Mei, 2023 ambapo timu maalumu ilifika uwandani mwezi Septemba, 2023 ili kubaini hali halisi wakati wa zoezi la uhakiki wa maeneo ya utawala.

Mheshimiwa Spika, ombi hili kwa sasa lipo katika hatua za mwisho za uhakiki wa vigezo na mrejesho utatolewa kabla ya mwezi Juni, 2024.