Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaupatia Mji wa Kibaha hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, ila kwa niaba ya Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, je, Serikali haioni haja sasa kufanya kwa haraka kwa sababu Mkoa wa Pwani umeanza mwaka 1972 na hauna hata halmashauri moja yenye hadhi, lakini pia Halmashauri ya Kibaha Mjini ina wakazi zaidi ya 200,000; lini kilio hiki kitazingatiwa kwa haraka? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali ni kuhakikisha inatekeleza suala hili kwa haraka zaidi, lakini kigezo kikubwa ni namna ambavyo halmashauri yenyewe inakidhi vigezo vya msingi vilivyowekwa ikiwemo idadi ya wananchi ambao hawapungui 300,000 lakini na vigezo vingine vingi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari timu yetu imeshafika uwandani kuona vigezo vingine na mwezi Juni mwaka huu tutaleta majibu ya hatua ambayo inafuata. Ahsante.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaupatia Mji wa Kibaha hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, Muleba ni moja ya miji yenye hadhi ya miji midogo tangu mwaka 2008. Ni lini itapata hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali ilishafanya tathmini kwenye Mamlaka za Miji Midogo kote nchini. Zipo mamlaka ambazo zinakidhi vigezo vya kupanda kuwa Halmashauri za Miji, lakini zipo mamlaka nyingi ambazo pia bado hazijakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi kuwa Hamashauri za Miji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kikoyo kwamba Halmashauri ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Muleba ni moja ya mamlaka ambazo zinafanyiwa tathmini ya vigezo na mara tutakapokuwa tumefanya tathmini na pale Serikali itakapokuwa ipo tayari kwa ajili ya kuanza kupandisha hadhi Mamlaka za Miji kuwa Halmashauri za Miji tutakwenda kufanya hivyo, ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaupatia Mji wa Kibaha hadhi ya Manispaa?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, Mlandizi ni Mamlaka ya Mji Mdogo tangu mwaka 2004 na Serikali inafahamu kuwa tunaenda kuujenga Mji wa Kwala, je, Serikali haioni sasa ni wakati sahihi kufanya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Vijijini kuwa Mji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mji wa Mlandizi unaendelea kukua kwa kasi kubwa, lakini ujenzi wa Mji wa Kwala utaongeza kasi ya ukuaji wa Mamlaka ya Mji wa Mlandizi pia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inalitambua hilo, na tayari imeshafanya hatua kadhaa kuelekea kuona vigezo kama vinafikia hatua inayotakiwa ili iweze kupandishwa hadhi ya kuwa Halmashauri au Manispaa, ahsante.