Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 11 Water and Irrigation Wizara ya Maji 139 2024-04-22

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, ipi kauli ya Serikali juu ya kutokamilika kwa Miradi ya Maji katika Jimbo la Kibamba?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha ujenzi wa miradi mitatu ya usambazaji wa maji kutokea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hadi Bagamoyo (2B-2F), Mshikamano na Kitopeni ambapo miradi hiyo inanufaisha wakazi wapatao 210,876 wa Jimbo la Kibamba.

Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa usambazaji maji Kusini mwa Dar es Salaam (Bangulo) ambapo utekelezaji wake umefikia 25% na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2024. Mradi huo ukikamilika utanufaisha wakazi wapatao 271,863 wa Jimbo la Kibamba.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kukamilisha utekelezaji wa miradi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Jimbo la Kibamba.