Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 141 2024-04-22

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji katika Bonde la Mto Kilombero?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2016 Serikali ilifanya upembuzi yakinifu wa awali (prefeasibility) wa miradi ya umwagiliaji katika bonde la Kilombero lenye ukubwa wa hekta 53,344 ambapo skimu za Kisegese, Udagaji, Mgungwe na Mpanga - Ngalamila zilihusishwa katika kazi hiyo. Upembuzi yakinifu wa awali ulibaini kuwa kuendelezwa kwa skimu hizo kutanufaisha kaya 15,102 na kutoa ajira 69,476.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina (feasibility study and detailed design) wa miradi ya umwagiliaji katika Bonde la Mto Kilombero kupitia Mshauri Elekezi ambaye yupo eneo la kazi. Baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, bonde hilo litaingizwa katika mpango wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji.