Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 376 2024-05-20

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza:-

Je, lini watumishi wa umma watarekebishiwa madaraja hasa walimu waliopandishwa na kunyang’anywa mwaka 2016 - 2018 kupisha uhakiki?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathani Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2016 Serikali ilisitisha mambo mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo upandishaji vyeo ili kupisha zoezi la uhakiki wa taarifa za kiutumishi na vyeti vya elimu kwa watumishi wa umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutatua changamoto zilizojitokeza kutokana na sitisho hilo mwaka 2021/2022 Serikali ilianza kutekeleza zoezi la kuwarejesha watumishi wa umma wa kada mbalimbali kwenye nafasi na vyeo vyao stahiki kwa njia mbalimbali ikiwemo msawazo wa vyeo na mserereko wa madaraja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla ya watumishi 375,904 wamepandishwa vyeo wakiwemo watumishi 85,471 walioathirika na zoezi la uhakiki. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali inatarajia kuwapandisha vyeo watumishi 81,503 wakiwemo walimu walioathirika na zoezi la uhakiki.