Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 381 2024-05-20

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza:-

Je, lini mradi wa ujenzi wa Feri ya MV Buyagu utakamilika ikizingatiwa kuwa mkataba wa ujenzi umekwisha muda wake Aprili, 2024?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inajenga kivuko kipya kitakachokuwa kiunganishi muhimu kati ya Wilaya ya Sengerema na Wilaya ya Misungwi kupitia eneo la Buyagu lililoko Sengerema na eneo la Mbalika lililopo Misungwi. Mkataba wa ujenzi wa kivuko hiki ulisainiwa mwezi Aprili, 2023 kati ya Serikali kupitia TEMESA na mkandarasi Songoro Marine Transport Mwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za ujenzi wa kivuko hiki zimepangwa kukamilika mwezi Agosti, 2024 baada ya muda wa awali kuongezwa, ahsante.