Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 382 2024-05-20

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kulipa fidia wananchi wa Kijiji cha Ngombo waliopisha Hifadhi ya Pori Tengefu la Kilombero?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Ngombo kipo katikati ya eneo la ardhi oevu ndani ya Pori Tengefu Kilombero. Uwepo wa kijiji hiki pamoja na vijiji vingine ndani ya pori hilo ulifanya ukubwa wa eneo la pori kupungua kwa 61.5% kutoka kilometa za mraba 6,500 hadi kilometa za mraba 2,500. Hali hiyo ilipelekea Serikali kupitia Kamati ya Mawaziri Nane kuelekeza Kijiji cha Ngombo kufutwa na wananchi wake kuhamishiwa maeneo mengine sambamba na eneo la Pori Tengefu Kilombero kupandishwa hadhi kuwa Pori la Akiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia hatua hiyo, Serikali imeshakamilisha zoezi la uthamini kwa wananchi wa Kijiji cha Ngombo kwa vitongoji vyote vitatu vinavyounda Kijiji hicho ambavyo ni Idenge, Ikwachu na Ifuru. Aidha, jumla ya shilingi 7,351,097,480.46 zimeainishwa kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi hao. Wizara inasubiri fedha kutoka Hazina ili iweze kulipa fidia kwa wananchi ili waweze kuondoka katika eneo la hifadhi na eneo hilo kuendelea kusimamiwa kama Pori la Akiba Kilombero kwa mujibu wa Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Sura ya 283.