Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza kulipa fidia wananchi wa Kijiji cha Ngombo waliopisha Hifadhi ya Pori Tengefu la Kilombero?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hawa wa Kijiji cha Ngombo wamekaa muda mrefu wakisubiri hiyo fidia ili waweze kuondoka kiasi ambacho wameshindwa kulima lakini pia wameshindwa shughuli nyingine zozote za kijamii ili kuweza kukidhi mahitaji yao na familia zao; je, nini kauli ya Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati kipindi hiki tunasubiri kupata fidia, je wananchi waendelee kuandaa mashamba yao ili kusudi waweze kujipatia chakula na kipato kwa ajili ya familia zao?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninawashukuru wananchi hawa kwa jinsi ambavyo wamekuwa na subira kuruhusu mchakato huu wa fidia ambao ni muhimu sana kufanyika uweze kukamilika. Nawaomba waendelee kuwa na subira, tunaamini ndani ya kipindi kifupi fidia hii itapatikana, kwa hiyo, wataendelea na maisha yao kama kawaida.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza kulipa fidia wananchi wa Kijiji cha Ngombo waliopisha Hifadhi ya Pori Tengefu la Kilombero?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, hivi sasa utaratibu wa fidia nchini kwa wanaoathiriwa na wanyama haueleweki vizuri. Serikali ina mpango gani wa kuweka wazi utaratibu huu wa fidia kwa wananchi wanaoathiriwa na wanyama katika mali zao na maisha yao?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, fidia kwa wananchi wanaopata madhara ya wanyama inafanyika kwa mujibu wa sheria na kanuni ambayo iko wazi na tumekuwa tukiisema mara kadhaa katika Bunge hili na kwa bahati nzuri kanuni hizi zimesambazwa kwa Maafisa Hifadhi wote wa halmashauri zetu ambao tunaamini na wao wanafanya kazi ya kutoa semina kwenye vijiji vyetu, lakini kama haieleweki natoa rai kwa Maafisa Wanyamapori katika halmashauri zetu waendelee kufanya kazi nzuri hii ya kutoa elimu kwa wananchi ili jambo hili lieleweke.