Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Water and Irrigation Wizara ya Maji 385 2024-05-20

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, lini kibali cha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu, Kamuli kitatolewa ili ujenzi uanze?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha za utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji utakaonufaisha vijiji 57 wilayani Kyerwa ikiwemo Kyerwa Mjini, Nyaruzumbura, Nyakatuntu hadi Kamuli kwa kutumia chanzo cha Mto Kagera. Aidha, katika mpango wa muda mfupi, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji itakayonufaisha vijiji 27 vya Nkwenda, Rwabwere, Karongo, Nyamiaga, Nyakatera, Kagu, Masheshe, Nyamweza, Kaikoti, Iteera, Muleba, Chanya, Kimuli, Rwanyango, Chakalisa, Kikukuru, Omukitembe, Karambi, Rwele, Rubilizi, Mukunyu, Kitwechenkura, Rukuraijo, Makazi, Kibimba, Nyakatete na Mabira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali katika mwaka wa fedha 2024/25 itachimba visima katika Vijiji vya Omuchwenkano, Businde, Nyaruzumbura, Bugara, Rukiri, Nyakatuntu, Kyerere, Kamuli, Ibamba na Rukuraijo ili kuongeza vyanzo vya maji. Kukamilika kwa miradi hiyo kutaboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji wilayani Kyerwa kufikia wastani wa 80.3% mwezi Juni, 2025. (Makofi)