Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, lini kibali cha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu, Kamuli kitatolewa ili ujenzi uanze?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kabla sijauliza maswali ya nyongeza, ninaomba nitoe pole kwa Wana-Kyerwa na Wizara ya Maji kwa kumpoteza Meneja wetu wa Wilaya, ndugu yangu Tungaraza, tunawapa pole sana Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niulize maswali mawili ya nyongeza; pamoja na Serikali kuweka mpango wa kuchimba visima vya maji, kuna visima ambavyo vimechimbwa zaidi ya miezi sita na mpaka sasa hivi visima hivi bado havijajengewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini visima hivi vitajengewa kwenye Kata ya Kibale, Kijiji cha Kigologolo, lakini pia kwenye Kata ya Businde, Kijiji cha Omuchwenkano?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna mradi wa maji katika Kata ya Songambele, Kijiji cha Songambele, ni zaidi ya mwaka sasa tumepitisha kwenye bajeti mradi huu haujaanza. Ni lini mradi mradi huu utaanza ili kuwapatia wananchi wa Songambele maji safi na salama? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kwa niaba ya RUWASA na Wizara ya Maji na sekta ya maji kwa ujumla tunapokea pole hizo kwa kuondokewa na DM wetu kutoka kule Kyerwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuhusu Kigologolo pamoja na Omuchwenkano, katika jibu langu la msingi nimeitaja Omuchwenkano, lakini vilevile katika Kigologolo, Serikali itaanza kwanza ukarabati kwa sababu ni kweli kabisa kisima kipo kimechimbwa, lakini bado ile miundombinu ya kusambazia maji haijakamilika na Serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba inafanya ukarabati wa miundombinu ili wananchi waweze kufikishiwa huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, katika mradi wa Songambele, kwanza nimpongeze sana kwa ufuatiliaji mzuri sana Mheshimiwa Innocent Bilakwate kwa ajili ya mradi huu na kwa ushirikiano ambao anaendeea kutupatia na sisi Serikali hatutamuangusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huu fedha ambazo zilitengwa kwa bahati mbaya au nzuri hatukuweza kuzipata kwa wakati. Nimhakikishie katika mwaka wa fedha 2024/2025 mkandarasi anaenda kupatikana na mradi huu utaanza mara moja, ahsante sana. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, lini kibali cha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu, Kamuli kitatolewa ili ujenzi uanze?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona, mwaka 2023/2024 Serikali ilitenga fedha kwa ajili ya mradi wa maji wa Kata za Itandula na Mbalamaziwa, Jimbo la Mufindi Kusini, lakini mpaka sasa fedha hizo hazijaenda. Ni lini Serikali itapeleka fedha hizo kukarabati mradi huo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua changamoto ya kucheleweshwa kufikishwa fedha katika mradi huo lakini nikuhakikishie kwamba kabla ya mwaka wa fedha haujaisha fedha hizo zitakuwa zimepelekwa, ahsante sana. (Makofi)