Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 550 2024-06-07

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta unafuu wa gharama za michango ya kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza na cha tano?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la 2023 ambalo pamoja na mambo megine inatamka kuwa Serikali itahakikisha kuwa elimu ya awali, msingi na sekondari inatolewa bila ada katika mfumo wa umma. Aidha, Waraka wa Elimu Na. 3 wa mwaka 2016 kuhusu utekelezaji wa Elimu Msingi Bila Malipo, unabainisha majukumu ya wadau wote ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kuzingatia ili kupata kibali cha mchango wa aina yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuleta unafuu wa gharama za michango, Serikali imetoa maelekezo ya kujiunga na kidato cha tano katika shule zote za sekondari za Serikali Tanzania ambapo ukomo wa michango hiyo umebainisha kuwa shilingi 80,000 kwa shule za bweni na shilingi 50,000 kwa shule za kutwa. Aidha, wanafunzi wa kidato cha kwanza wanapokelewa kwa kuzingatia Waraka wa Elimu Na. 3 wa mwaka 2016 wa Elimu Msingi bila Ada ambapo wanafunzi hawatakiwi kutoa mchango wowote bila kibali cha Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya.